December 5, 2014

NYOSSO (KUSHOTO) WAKATI AKIITUMIKIA COASTAL. KULIA NI DAVID LUHENDE ALIYEKUWA YANGA, SASA YUKO MTIBWA.
Baada ya kukaa nje ya Ligi Kuu Bara kwa miezi mitano, hatimaye beki wa kati, Juma Nyosso, amerejea kazini na kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia Mbeya City ya jijini Mbeya.


Nyosso baada ya kumaliza mkataba wa kuitumikia Coastal Union ya Tanga msimu uliopita, hakuwa na timu, alikuwa akihusishwa kurejea Simba lakini imekuwa tofauti.

Taarifa kutoka kwa mtu wa karibu na mchezaji huyo zinasema alishasaini na tayari yupo Mbeya kwa ajili ya kazi.

Kuhusiana na hilo, Nyosso na alisema: “Ndiyo nipo Mbeya, nimeshasaini mwaka mmoja na hapa nipo kwenye mazoezi binafsi ila tutaongea vizuri baadaye.”


SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic