July 18, 2015


Mwanasiasa maarufu wa Kenya, Raila Odinga leo anatarajiwa kushuhudia mechi ya ufunguzi ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame itakayozikutanisha Yanga na Gor Mahia ya Kenya kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Odinga ambaye ni kiongozi wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM)’ ni shabiki mkubwa wa Gor Mahia atakuwa sambamba na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo waliosafiri kutoka Kenya kuja kuishangilia.
ODINGA...

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, Odinga ambaye anayedaiwa kuwa na urafiki na Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, atatazama mechi hiyo kisha atakutana na baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara wa Tanzania.

Urafiki wa Magufuli na Odinga umethibitishwa zaidi hivi karibuni ambapo waziri huyo aliyechaguliwa kuwania urasi wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwenda Kenya katika mazishi ya mtoto wa Odinga pia aliwahi kumuunga mkono katika kampeni za urais.

Pamoja na urafiki wake na Magufuli, Odinga ni rafiki wa karibu wa Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ambaye imeelezwa huenda akaungana nao uwanjani katika mechi hiyo.

Manji aliwahi kumualika Odinga wakati wa ufunguzi wa maduka yake makubwa ya kibishara ya Quality Centre jijini Dar es Salaam.


Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mchezo huo bila shaka ataiunga mkono Yanga ambayo ni Tanzania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic