July 18, 2015


Mshambuliaji mwenye minguvu wa Simba, Elius Maguli, ameonekana kujiamini kupitiliza baada ya kutamka kuwa atafanya kazi yake kwa ufasaha na kuwazidi ujanja Laudit Mavugo na Khamis Kiiza ili yeye awe bora zaidi yao.

Maguli ameenda mbali zaidi kwa kusema, yeye ndiye mbadala wa straika Emmanuel Okwi aliyejiunga na Klabu ya Sonderjyske ya Denmark na siyo mchezaji mwingine yeyote.

Tayari Kiiza ameshajiunga na Simba lakini Mavugo bado yupo kwao akimalizia mechi za timu yake ya Vital’O ndipo aje nchini kujiunga na Wekundu wa Msimbazi.

Maguli alisema haangalii rekodi bali anasubiri kuona uwezo utakaoonyeshwa na wachezaji hao na atapambana nao kwa kufanya mazoezi ya nguvu kuwapiku.

“Unadhani nitaangalia eti nani kafanya nini? Siogopi lolote kwa hao jamaa ninaogombea nao namba, mimi nitapambana kwa mazoezi binafsi na tukikutana kwenye mazoezi ya wote watauona moto wangu,” alisema Maguli.

Hadi sasa Mavugo anaelezwa kufunga mabao 34 katika msimu unaomalizika huko Burundi katika michuano yote na uwezo wa kufunga wa Kiiza unafahamika tangu alipokuwa Yanga msimu uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic