April 4, 2016


Baada ya kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (FA), kocha mkuu wa timu ya Mwadui ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ametamka kuwa lengo lake kubwa ni kuona kikosi hicho kinatwaa ubingwa wa kombe hilo na kwenda kuiwakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho.

Mwadui imefanikiwa kutinga nusu fainali baada ya kuiondosha Geita Gold inayofundishwa na kocha wa zamani wa Simba, Seleman Matola, ambapo sasa wanasubiri kuchuana na Yanga, Azam au Coastal Union au Simba.

Julio alisema kuwa sababu kubwa ya kulipigia hesabu kombe hilo la shirikisho ni kiu yake ya kuona kikosi hicho kinapata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya kimataifa.

“Sisi hatuogopi timu yoyote ile ambayo tutapangiwa kwenye mashindano haya maana malengo yetu ni kuhakikisha tunatwaa ubingwa wa kombe hili na tuna kila sababu ya kufanya hivyo kutokana na uimara wa kikosi changu ambacho kinaweza kucheza na Yanga au Azam na tukawafunga.


”Tunalitolea macho kombe hilo kutokana na kutaka kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa,” alisema Julio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic