November 2, 2016



MPIRA UKWISHAAAAA
-Mnyate anaachia shuti la chinichini hapa lakini ni goal kick
-Mpira unateleza na unaonekana kuwasumbua wachezaji wengi
-Simba wanaonekana kuosha kila mpira unaokwenda langoni mwao
DAKIKA 6 ZA NYONGEZA
Dk 89, Simba wanapata kona na inakwenda kuchongwa Bukungu, kipa Frank Muonge anajitahidi kudaka vizuri kabisa
SUB Dk 88, Ibrahim Ajibu anaingia kuchukua nafasi ya Mavugo
Dk 88, mvua imeanza kunyesha uwanjani hapa na mashabiki wengi wanakimbia kutoka majukwaani
Dk 87, Angban yuko chini baada ya kuumia wakati akijaribu kuudaka mpira wakati wa shambulizi lililoelekezwa langoni mwake

Dk 82, kipa Muhonge anatoka na kumuwahi Mavugo aliyekuwa anakaribia kufunga. Lakini anampiga na mguu tumboni wakati akiokoa
Dk 81, Mavugo anapokeza nafasi mujarab ya kufunga kwa kuwa kipa wa Stand alikuwa ametoka langoni, likiwa wazi MAvugo amepiga nje
SUB 80, Moussa Ndusha ambaye ITC yake imekuja, anaingia kuchukua nafasi ya Kazimoto
SUB Dk 75 Kichuya anatoka na nafasi yake inachukuliwa na Jamal Simba Mnyate

DK 70, Wanachofanya Simba, wote wamerudi nyuma na wanafanya mashambulizi kwa kuwatumia watu watatu waende mbele kushambulia ambao ni Kichuya, Mavugo na Mwinyi Kazimoto tu
Dk 67, Kiemba anafanya yake hapa, anamtoka Bukungu na Juuko na kutoa pasi safi

Dk 64, Mo Ibrahim anaingia vizuri, ananyoshaa, unapita juu kidogo
DK 60, Selembe anapiga kichwa safi mbele ya mabeki wa Simba, goal kick
Dk 58, Stand wanapata kona inachongwa na Angban anaidaka kwa ulaini kabisa
Dk 56, Job analazimika kufanya kazi ya ziada kuokoa pasi nzuri ya Kichuya iliyokuwa inakwenda kwa Mo Ibrahim. Inakuwa inachongwa lakini haina faida
Dk 53, Stand wanafanya shambulizi kwa mpira wa adhabu, lakini juuuu
Dk 50, Stand wanaonekana kwenda taratibu na zaidi wanamtumia Amri Kiemba ambaye yuko vizuri
Dk 47, mpira umeanza kwa kasi na Stand United wanaonekana wamepania kusawazisha bao


DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
Dk 45, Kichuya anapaa kama mkizi na kuunganisha kichwa mpira wa adhabu lakini unatoka sentimeta chache kwenye lango la Stand
Dk 43, hakuna shambulizi kali zaidi ya kila timu kupiga pasi nyingi, Stand wakionekaan kufika zaidi kwenye lango la Simba
Dk 42 sasa, Stand wanaonekana kuongeza mashambulizi mengi zaidi ya Simba ambao wanafanya mashambulizi ya kushitukiza tu
Dk 35, Stand wanapata kona baada ya kusukuma mashambulizi mfululizo kwenye lango la Simba
]Dk 33, GOOOOOOOOO Kichuya aaukwamisha mpira wavuni
Dk 31, PENAAAAAAAT...MAVUGO Anaangushwa na Adeyum
Dk 30, Stand wanafanya shambulizi kali hapa, piga nikupige lakini Simba wanaokoa
KADI Dk 29, Mwanjale analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Sabato
Dk 27, mpira unaendelea lakini ni taratibu kutoka kila upande kama vile hakuna timu yenye haraka
Dk 26 sasa, mpira umesimama, kuna mchezaji wa Stand United anatibiwa pale uwanjani
Dk 23, Mo Ibrahim anapoteza nafasi nzuri hapa ya kufunga akiwa amebaki na lango, mpira unamzidi nguvu
Dk 22, mpira unaonekana kuchezwa zaidi katikati ya uwanja na hakuna mashambulizi makali kwenye milango
DK 19, Bukungu anafanya kazi ya ziada kuokoa krosi ya Kelvin Sabato
Dk 13, Stand wanaonekana ni wengi zaidi nyumba huku wakifanya mashambulizi ya kushitukiza
Dk 10, mpira unaonekana kuwa wa juu zaidi na hata milango haina kashkash sana, kila timu iko makini kwenye ulinzi
Dk 5 sasa, bado mpira unaonyesha kuchangamka lakini timu zote mbili si bora katika umaliziaji
Dk 1, mechi inaanza na Simba wanakuwa wa kwanza kushambulia. Lakini Mavugo anacheza faulo na mwamuzi anasema mpira uelekezwe Simba

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic