February 28, 2013





Mwanariadha maarufu wa Jamaica, Usain Bolt anatarajia kuweka rekodi mpya ya malipo pale atakaposhiriki mashindano ya Diamond League yatakayofanyika katika kipindi cha joto jijini Paris, Ufaransa.

Waandaaji wametangaza kuwa Bolt atalipwa dola 10,000 (Sh milioni 16) kwa kila sekunde wakati akikimbia mbio za Mita 200, Julai 6, mwaka huu.
Maana yake, Bolti anatarajia kuingiza hadi dola 200,000 (zaidi ya Sh milioni 160) katika mashindano hayo aliyokuwa hajashiriki tokea mwaka 2009.

Bolt alikuwa ameamua kujitoa kushiriki mashindano karibu yote ya Ulaya kutokana na kukatwa kodi kubwa kila anapokuwa anapokea malipo. Safari hii, waandaaji walifanya mazungumzo na serikali ya Ufaransa na kufikia makubaliano ya kuondoa kodi hiyo.

Kwa malipo hayo, yanamfanya kuwa mwanarisha anayelipwa fedha nyingi zaidi kuliko mwingine yoyote pia mwanamichezo kwa ujumla anayelipwa kitita kikubwa zaidi katika kipindi kifupi cha ushiriki wake wa michezo.

Mwanariadha huyo mwenye kasi kuliko mwingine yoyote duniani pia anatarajkia kushiriki katika mbio za London Grand Prix zitakazofanyika Julai 27 hasa kama suala la kodi litafanyiwa marekebisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic