February 28, 2013




Pamoja na kuonekana haina nafasi ya kutosha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England, Chelsea imeendeleza mbio za kutaka kutwaa kikombe cha FA baada ya kuichapa Middlesbrough maarufu kama Boro kwa mabao 2-0.

Chelsea waliokuwa wageni katika Uwanja wa Riverside, walikwenda mapumziko wakiwa hawana bao kama ilivyokuwa kwa wenyeji wao.



Kwa ushindi huo, Chelsea imefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali na sasa itakutana na Man United.
 

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Chelsea wakipeleka mashambulizi mfululizo hadi walipopata bao katika dakika ya 51 kupitia Ramires aliyepokea pasi ya Hazard ambaye kabla aliwahadaa walinzi. Shuti lake lilimgonga mgongoni Torres na kumpoteza kipa wa Boro.

Wenyeji walionekana kuchanganyikiwa, hata hivyo baadaye walichangamka na kuanza kusukuma mashambulizi mfululizo na kuifanya Chelsea kuwa katika wakati mgumu.
Wakati ikionekana kama Middlesbrough walikuwa wanakaribia kusawazisha, Chelsea walipata bao la pili katika dakika ya 73 kupitia kwa Moses.

Bila ya ubishi, pamoja na kujaribu lakini ilionekana wenyeji hawakuwa na njia tena ya kuing’oa Chelsea isisonge mbele katika michuano hiyo ya Kombe la FA ambayo ina heshima kubwa nchini England.

VIKOSI:
Middlesbrough: Steele, Bailey, McManus, Bikey (Hines 35), Friend, Carayol (Zemmama 74), Leadbitter, Rhys Williams, Haroun, Main (Miller 62), McDonald.
Subs: Leutwiler, Emnes, Ledesma,  Smallwood.


Chelsea: Cech, Ferreira, Ivanovic, Terry, Bertrand, Ake, Ramires, Moses (Luiz 76), Oscar (Marin 79), Benayoun (Hazard 58), Torres.
Subs: Turnbull, Cole, Lampard, Ba.

Mabao: Ramires 51, Moses 73.

ROBO FAINALI

Everton v Wigan
Manchester City v Barnsley
Millwall v Blackburn Rovers
Manchester United v Chelsea

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic