Kocha wa zamani wa Simba, Milovan
Cirkovic amesema fedha dola 35,000 (zaidi ya Sh milioni 55) alizolipwa na
Malkia wa nyuki zimeingia katika akaunti yake nchini Serbia.
Milovan raia wa Serbia amesema
fedha hizo tayari zimeingia ikiwa na maana tayari amepata malipo yake na
ameshamalizana na Simba.
“Kila kitu kipo safi,
nimewasiliana na mke wangu na kanihakikishia kwamba fedha zimeingia katika
akaunti yangu. Kwanza nianze kumshukuru Malkia wa nyuki.
“Kutokea kwa huyo mama (Malkia wa
Nyuki) imekuwa ni ahueni kwangu, nimeshukuru sana nimemalizana na Simba vizuri
na ndicho nilitaka kwa kuwa nina marafiki wengi hapa, sikutaka hadi tufikie
kushitakiana.
“Lakini nilikuwa sina ujanja,
ilikuwa lazima nifanye hivyo. Lakini mama ameokoa mambo, nafurahi pia
nawashukuru Wanasimba wote kwa kuniunga mkono tokea nikiwa kocha hadi
nilipokuja kudai fedha zangu,” alisema.
Milovan anatarajia kuondoka nchini
ndani ya siku mbili tokea leo kurejea kwao Serbia ambako atasubiri maombi ya
kuzifundisha timu ambazo zitakuwa zimevutiwa naye.
Malkia wa Nyuki alijitokeza
kumlipa Milovan baada ya uongozi wa Simba kuonekana ukisuasua kufanya hivyo
licha ya kumpa ahadi kibao za kumaliza suala hilo, bila ya mafanikio.
Milovan alikuwa anadai dola 32,000 lakini Malkia wa nyuki alimlipa zaidi dola 3,000.
simba mnatuabisha bhana malkia badala ya kufanya vitu vingine vya ndani ya klabu yeye analipa madeni jamani hebu kuweni na akili siku nyingine mtakosa wakujitolea kwaasababu ya uzembe
ReplyDelete