Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji
amesema presha yake kubwa imehamia katika mechi ya Jumamosi pale vijana wake
watakapoivaa Kagera Sugar.
Manji amesema presha imekuwa juu
kwa zaidi ya siku tatu kabla ya kuivaa Azam FC kwa kuwa ulikuwa ni mchezo
muhimu sana na walitaka ushindi.
“Nafurahi vijana wamefanya vizuri
na kushinda bao moja, kikubwa kwetu kilikuwa ni pointi tatu kwa kuwa ulikuwa ni
mchezo muhimu sana.
“Ajabu sasa naona presha imerudi
palepale na imehamia kwa Kagera Sugar, nataka kushinda kila mechi lakini ligi
ni ngumu na upinzani uko juu sana.
“Lakini ninaamini tunaweza kufanya
vizuri kwa kuwa wachezaji wamekuwa wakionyesha juhudi na viongozi wanafanya
jitihada katika kuhudumia timu,” alisema.
Yanga ina pointi 39 kileleni,
iwapo itaishinda Kagera Sugar keshokutwa, itakuwa imejiweka katika mazingira
mazuri ya kutwaa ubingwa ambao watetezi wake Simba wanaonekana kusuasua.
0 COMMENTS:
Post a Comment