Kama
unakumbuka Mtibwa Sugar ndiyo waliokuwa wa kwanza kuwafunga Simba katika
mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara.
Baada
ya kuwafunga kwa mabao 2-0 mjini Morogoro, tafrani kubwa likazuka mashabiki
wakitaka kipa Juma Kaseja na Makamu Mwenyekiti, Geofrey Nyange ‘Kaburu’
waondoke.
Baada
ya hapo, Simba ikapoteza mechi ya pili dhidi ya Toto African kwa kufungwa bao
1-0, safari hii nyumbani Taifa.
Tokea
kuanza kwa mzunguko wa pili, Simba haijapoteza hata mechi moja, kwani baada ya
kucheza nne, imeshinda mbili na sare mbili. Sasa inakutana tena na Mtibwa Sugar,
nini kitatokea?
Inawezekana
kwa Simba kukubali kuwa wateja wa Mtibwa Sugar msimu huu? Au ndiyo wakati
mwafaka kwa mabingwa hao watetezi kulipa kisasi kwa ‘Wakata miwa’ wa Manungu?
Hakuna
ubishi mchezo utakuwa mgumu kwa kuwa kati ya timu hizo mbili, hakuna kikosi
legelege ingawa Mtibwa iliwashangaza wengi hivi karibuni, kwani baada ya
kuwakomalia Yanga kwa sare ya bao 1-1, ikalala kwa Azam FC kwa mabao manne!
Katika
mechi ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar. Mtibwa Sugar iliyo katika nafasi ya
saba na pointi 24, itakuwa inapambana kukwekea juu wakati Simba yenye 31
inataka kuifukuza Azam FC yenye 36.
Ngome ya Mtibwa imeruhusu mabao 18 ambayo ni mengi zaidi ya ngome ya Simba ambayo imefungwa mabao 14.
USHAMBULIAJI:
Simba
imefunga mabao 26, huku Mtibwa ikiwa imepata 20 tu hali inayoonyesha Msimbazi
ni imara zaidi kama litakuwa ni suala la takwimu.
Lakini
bado Mtibwa Sugar inaonekana ni moja ya timu zinazoonyesha soka la uhakika
ikiwa chini ya wazalendo Mecky Maxime, Zuberi Katwila na Patrick Mwangata
wakati Simba inayonolewa na Mfaransa Patrick Liewig akisaidiwa na Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’ bado haijaonyesha kiwango kinachowaridisha mashabiki wake.
Dakika
90 za leo ndiyo zitatoa matokeo lakini iwapo mshambuliaji Felix Sunzu atakuwa
amepona na kuongeza nguvu basi Simba itakuwa hatari zaidi wakati Hussein Javu na
Shaban Kisiga ni wachezaji wa kuchungwa sana na walinzi wa Simba, la sivyo
watalia.
Kipa
wa Mtibwa Sugar, Casillas huenda akawa mmoja ya wachezaji kivutio kutokana na
umahiri ambao amekuwa akiuonyesha hivi karibuni katika mechi mbalimbali za
ligi.
0 COMMENTS:
Post a Comment