Mourinho ataka
mwamuzi wa El Classico aachwe
Kocha Mkuu wa Real Madrid, Jose Mourinho ametaka
mwamuzi atakayechezesha mechi ya leo usiku dhidi ya Barcelona aachwe kabisa.
Katika mechi hiyo maarufu kama El Classico, Mourinho
amesema wamejifunza mengi kuhusiana na mwamuzi walipokutana na Barcelona na akaonya wapinzani wake hao waachane na kuzungumzia kuhusiana na mwamuzi.
Lakini akaonya kwamba amesikia Barcelona wakizungumzia
kuhusiana na mwamuzi, kitu anachoamini ni vizuri kila timu ikajipanga kucheza
soka leo.
“Sidhani kama ni sahihi, kuanza kuwaza namna ya
kusababisha upande mmoja upate kadi, badala yake tucheze soka. Ingawa tuliitaka
sana mechi na Barcelona, lakini tuna jukumu zito tena dhidi ya Man United. Tunajua
ni kazi ngumu lakini tutapambana.
“Mwamuzi awe mwenye haki na aachwe afanye kazi yake,
mimi najua itakuwa ni mechi ngumu na gumzo,” alisema Mourinho.
Messi: Kelele
zao hazitanichanganya
Mshambuliaji nyota wa Barcelona, Lionel Messi amesema wale
wanaomlaumu kamwe hawawezi kumchanganya kabla ya kuwavaa Madrid leo.
“Najua kuna mechi ngumu mbele yetu, tunacheza na Real
Madrid, timu yenye wachezaji bora na iliyokamilika kifiziki.
“Kupambana nao inataka ufundi, moyo wa kujituma na
kupania kushinda. Lakini wanaolaumu hasa katika kipindi hiki, nafikiri wanataka
kunichanganya. Watakuwa wanajidanganya, mimi na wenzangu tumeelekeza nguvu
katika mechi hiyo,” alisema Messi.
“Mechi kama mbili hatukuwa katika kiwango kizuri,
hatuna ujanja lazima turudi katika mechi dhidi ya Madrid, pia ni vizuri
tushinde.”
Wachezaji Madrid
kufika Barcelona siku ya mechi
Kikosi cha Real Madrid kitatua leo mjini Barcelona kwa
ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Mfalme, baada ya sare katika mechi ya
kwanza mjini Madrid.
Uamuzi wa Madrid kutua leo na kuivaa Barcelona, kidogo
umewashangaza wengi kwa kuwa hii ni mara ya kwanza mambo kwenda hivyo lakini Kocha Jose Mourinho anaamini ni uamuzi sahihi.
Wachezaji wa Madrid watapumzika hotelini kwa muda
mchache kabla ya kwenda uwanjani kwa ajili ya mechi hiyo inayosubiriwa kwa
hamu.
Pamoja na hivyo, Mourinho amewashangaza wengi zaidi
baada ya kufanya mazoezi na kikosi chake katika eneo la Valdebebas mjini Madrid
na baada ya mazoezi akawaruhusu wachezaji kulala makwao.
Higuain kuanza,
Kaka, Di Maria kugombea namba
Hadi jana usiku ilikuwa haijajulikana wachezaji 11 wa
Real Madrid watakaoanza katika mechi ya leo ya Kombe la Mfalme dhidi ya
Barcelona.
Jose Mourinho amesema hana uhakika ingawa dalili
zinaonyesha ataanza na Higuain huku wawili, Ricardo Kaka aliyerejea uwanjani
ana Angelo Di Maria wakigombea kuanza.
Mourinho ametamba kwamba katika kikosi chake kila
mchezaji yuko fiti na anataka kucheza mechi hiyo, kitu ambacho ni bora kwake.
Mourinho amesema wachezaji watatangaziwa kikosi leo,
ingawa amekwishawaeleza kila mmoja kujiandaa kwa kuwa yoyote anaweza kucheza
tofauti na watu wanavyofikiria.
Fabregas: Hatuchongi sana kwenye vyombo vya habari
Kiungo wa Barcelona, Cecs Fabregas amesema wachezaji
wa Barcelona hawana tabia ya kuzungumza sana na kulaumu kwenye vyombo vya
habari.
Fabregas amewaambia waandishi wa habari kwamba
wasingependa kuzungumza sana kuhusiana na mechi yao ya leo ya Kombe la Mfalme,
badala yake watatoa majibu uwanjani.
Akizungumza kuhusiana na mchezo huo unaosubiriwa kwa
hamu, Fabregas alisema wao wako katika hali nzuri na wanataka kucheza.
“Mfano mzuri unaweza kuwa Messi, unaona hazungumzi
sana katika mikutano ya waandishi lakini majibu yake uwanjani.
“Anataka kucheza pia kushinda lakini kuinyoi mpira pia
ni kitu muhimu. Hivyo subirini uwanjani tutafanya kazi yetu,” alisema Fabregas.
0 COMMENTS:
Post a Comment