Baada ya mashabiki wa Man United kuingia hofu kutokana
na kuumia kwa mshambuliaji wao, Robin van Persie, sasa mambo yanaonekana kuwa ‘mswano’.
Van Persie alitolewa nje katika mechi ya Premiership
wakati Man United ilipoivaa QPR baada ya kuumia karibu na kiuno baada ya
kuanguka na kuigonga kamera, hali iliyozua hofu.
Lakini jana Jumatatu alionekana katika mitaa ya Alderley
Edge akiwa na mpenzi wake, tena alionyesha kutokuwa na dalili yoyote ya
maumivu.
Hali hiyo inaashiria Man United itakuwa na van Persie
katika mechi yao muhimu ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya mabingwa wa
Hispania, Real Madrid siku chache zijazo.
Van Persie alipoulizwa kuhusiana na maumivu aliyokuwa
nayo, alijivu kwa kifupi tu: “Nidyo, kila kitu kipo safi, namshukuru Mungu.”
Baada ya hapo, alitembea hatua chache na kuingia
katika gari lake la kifahari aina ya Porsche na kuondoka zake.
Mholanzi huyo ndiye tegemeo la mashambulizi katika
kikosi hicho cha Alex Ferguson na kawaida humpanga na Wayne Rooney, hali
inayoifanya Man United kuwa tishio tokea kuanza kwa msimu huu.
VAN PERSIE AKIONDOKA ZAKE...
0 COMMENTS:
Post a Comment