March 12, 2013



Mmoja wa viungo bora waliowahi kutokea nchini England, Paul Gascoigne amerejea nchini humo na kusema Kocha Mkuu wa Manchester United, Alex Ferguson na mshambuliaji wake, Wayne Rooney wamesaidia kuokoa maisha.

Mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham na timu ya taifa ya England, alikuwa Arizona nchini Marekani kwa wiki tano akiwa anapata tiba maalum.


Gascoigne maarufu kama Gazza alisema Ferguson alimtumia ujumbe na kumtaka aendelee kupambana na maisha yake ya sasa kwa kuwa sima mazuri.

“Ferguson aliniambia anatambua mimi ni mpambanaji, hivyo sipaswi kukata tamaa. Alisisitiza niendelee kupambana na mambo yatakuwa mazuri,” alisema Gazza mwenye umri wa miaka 45.

“Pamoja na kuniambia maneno mengi ya upendo, Ferguson alisisitiza alikuwa akizungumza kwa niaba ya wachezaji wote wa Man United. Kweli imenifariji sana.
“Lakini Rooney alijirekodi na kunitumia ujumbe wa picha, alinieleza anavyovutiwa na mimi na anavyoamini nitarejea katika hali yangu nzuri.

“Alisema siku akiwa na nafasi, atanialika ili niende kujumuika na wachezaji kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kabla ya mechi.”

Gazza amekuwa akisumbuliwa na ulevi wa kupindukia, hali inayomlazimu kupata tiba maalum ili kupunguza unywaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic