March 6, 2013




Kiungo mzoefu wa vinara wa Ligi Kuu BaraYanga, Nurdin Bakari atafanyiwa upasuaji wa goti wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya amethibitisha hilo leo, mara tu baada ya mazoezi ya timu hiyo leo kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama.

Nurdin ambaye alijiunga na Yanga akitokea Simba misimu minne iliyopita, amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti kwa muda mrefu sasa.

“Imekuwa ni muda sasa, lakini katika mazoezi ya jana alijitonesha tena. Kocha akataka kujua, mwisho tukashauriana kuwa ni bora kulimaliza kama hilo tatizo na matibabu sahihi ni upasuaji,” alisema Matuzya aliyechukua nafasi ya Juma Sufiani.


Nurdin (kulia) mazoezini jana...
 
Vipimo vya goti la Nurdin kesho vitawasilishwa katika hospitali ya Mwananyamala, baada ya hapo itapangwa hospitali ambayo atafanyiwa upasuaji huo, wiki ijayo.
Katika siku za hivi karibuni, kiwango cha Nurdin kimeporomoka na imeelezwa majeruhi hayo yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa.

Nurdin ni kati ya wachezaji wenye uwezo wa kucheza namba nyingi uwanjani kama mbili, tatu, nne, tano, sita, saba tena kwa ufasaha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic