March 6, 2013



 *Wamfuata airport, yeye agoma kujibu maswali yao
Waandishi Waingereza waliamka alfajiri na mapema siku iliyofuata baada ya Man United kutolewa na Real Madrid na kufunga safari hadi Uwanja wa Ndege wa Manchester ili kuzungumza na mwamuzi Cuneyt Cakir.

Cakir raia wa Uturuki, hakuwa tayari kuzungumza lolote pamoja na waandishi hao kuwa wamemuandalia maswali. Akiongozana na wenzake wanne, aliwaacha solemba.
Hasira za waandishi hao zikamalizikia kwenye uchunguzi na kugundua Cakir amekuwa mahiri kwa kutoa kadi katika mechi za Ligi Kuu ya Uturuki na anasifika kwa kuboronga mechi zake.




Pia walionyesha ambavyo amekuwa mmoja wa marafiki wa Ronaldo wa real Madrid katika mtandao wa kijamii wa Twitter, wakianisha kama moja ya vigezo vya Cakir kuboronga mchezo huo wa hatua ya 16 Bora ambao ulimalizika kwa wageni Real Madrid kushinda kwa mabao 2-1, la ushindi likiwa limetupiwa na Ronaldo.

Cakir alimtwanga Nani wa Man United kadi nyekundu moja kwa moja baada ya kumkanyaga Arbeloa wa Real Madrid, lakini mjadala umekuwa mkubwa wengine wakiamini mwamuzi huyo hakuwa sahihi.

Mjadala ni mkubwa kwa kuwa wako wengi wanaopinga, lakini wako wamekuwa wakisisitiza kwamba Cakir alikuwa sahihi kumpa kadi hiyo Nani, kwani pamoja na kutomuona Arbeloa, baadaye aliongeza kumkanyaga kwa makusudi.

Rekodi zilizopatikana zimeonyesha Cakir hajawahi kuchezesha mechi yoyote bila ya kutoa kadi. Inaelezwa tokea Januari, mwaka huu tayari alikuwa ametoa kadi 36 za njano, tatu nyekundu. Hizo amemwaga katika mechi nane tu za ligi alizochezesha.

Mechi yake ya mwisho ya ligi kwao Uturuki kabla hajafunga safari kwenda Uingereza kuchezesha mechi hiyo katika Man United dhidi ya Real Madrid, Cakir  alimwaga kadi sita za njano katika mechi hiyo iliyowakutanisha Akhisar Beledi dhidi ya Elazigspor.

Waingereza hao wamezidi kuangusha makombora kwamba Cakir hajawahi kupewa mechi kubwa msimu huu, mara ya mwisho ilikuwa mechi ya Super Cup kati ya vigogo wa Uturuki, Galatasaray dhidi ya Fenerbahce, Agosti, mwaka jana.

Uthibitisho yeye ni rafiki wa Ronaldo kwenye Twitter...


MASWALI ALIYOANDALIWA AKAGOMA KUYAJIBU:
  1. Unafikiri ulifanya vizuri kazi yako siku ya mechi?
  2. Unajuta kutokana na kadi uliyompa Nani?
  3. Ferguson alikuambia kitu kipi wakati wa dakika zote za mchezo?
  4. Je, unatarajia kurejea Old Trafford?
  5. Je, unatarajia kupata kadi ya Krismas kutoka kwa Rio Ferdnand?
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic