March 12, 2013




Wakati inaendelea kupambana kuokoa roho yake, ili ibaki katika Ligi Kuu England, klabu ya Reading imetangaza kumtimua kazi kocha wake mkuu, Brian McDermott.
Readind iliendelea kudidimia katika msimamo wa Premiership baada ya kufungwa mabao 2-1 na Aston Villa, Jumamosi iliyopita.

Imeelezwa, McDermott amechanganikiwa na uamuzi huo wa klabu baada ya siku 33 zilizopita kufanikiwa kutangazwa kocha bora wa Premiership.


Muitaliano Paolo Di Canio anaelezwa ni kati ya wanaopewa nafasi ya kuwa makocha wa Reading na Jumamosi alikuwa uwanjani wakati Reading ikipambana na Aston Villa.
Mmiliki wa Reading, Anton Zingarevich alitoa shukurani kwa kocha huyo ambaye amekuwa na mafanikio makubwa katika klabu hiyo tokea alipoanza kuifundisha mwaka 2009.

Brian aliisaidia Reading kupanda daraja hadi Premiership ikiwa ni mara ya pili katika historia ya klabu na inaonekana kutokana na mambo yanavyokwenda, klabu hiyo haiwezi kukwepa kuteremka.

Premiership ina timu 20 huku Reading ikiwa katika nafasi ya 19 na pointi 23 sawa na QPR inayoburuza mkia.

McDermott amewahi kuichezea Arsenal katika mwanzo mwa miaka ya 1970 akiwa mmoja wa viungo mahiri, baadaye akajiunga na Fulham.

Msimu wa 2011-12 alionyesha ni mmoja wa makocha bora baada ya kuipa timu hiyo ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza England maarufu kama Championship.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic