March 9, 2013




Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Simba, Rahma Al Kharusi maarufu kama Malkia wa Nyuki amesema Simba inapaswa kujipanga kwa ajili ya msimu ujao.

Malkia wa Nyuki amesema kimahesabu inaonekana Simba imepotea lakini haitawakatisha tama kuhakikisha inafanya vizuri angalau mechi zilizobaki.


“Lazima tuwe waungwana na kuangalia hali inavyokwenda, Simba haiku vizuri na mambo mengi hayakwenda vizuri lakini hatuwezi kukata tamaa na kuacha kila kitu kiende hovyo.

“Ninaamini tukishirikiana tunaweza kumaliza mambo angalau vizuri na msimu ukaisha tukiwa na nafasi nzuri hata kama tutakuwa tumekosa ubingwa. Lakini msimu unaokuja ndiyo tunatakiwa kuulenga.

“KIla kitu tunatakiwa kufanya mapema ili kujipanga vizuri, utaona mambo kidogo si mazuri ndani ya klabu lakini Wanasimba wanapaswa kuwa na subira na kujipanga ili mambo yarekebishwe,” alisema Malkia wa Nyuki.

Wiki iliyopita, Malkia wa Nyuki aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Simba lakini siku chache baadaye, makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ akajiuzuru nafasi ya umakamu mwenyekiti wa Simba.

Lakini kabla ya hapo, mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo, Zacharia Hans Pope ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili naye akabwaga manyanga.
Mashabiki wamekuwa wakisubiri kwa hamu kuona Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage ambaye yuko katika matibabu nchini India naye anabwaga manyanga.

Simba ambao ni mabingwa watetezi wamekuwa wakisuasua katika nafasi ya tatu wakati Yanga na Azam FC ndiyo wanaoonekana wametulia zaidi katika mbio za kuwania ubingwa huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic