March 10, 2013




Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji hatimaye ameamua kusema ukweli anavyojisikia kuhusiana na Ligi Kuu Bara inavyokwenda ukingoni.

Manji amesema amekuwa na presha kubwa kupindukia kadri Ligi Kuu Bara inavyokwenda ukingoni hali inayomyima raha.

Akizungumza na Salehjembe, Manji amesema wakati mwingine analazimika kusimamisha shughuli zake nyingine Yanga inapokuwa uwanjani.


“Kweli kuongoza ni kazi kubwa, kila mechi unataka kushinda. Nilisema dhidi ya Azam FC ilikuwa ni muhimu zaidi, lakini baada ya hapo nikaona dhidi ya Kagera ni ngumu zaidi.

“Nayo ikapita, kama tumeshamaliza lakini inaonekana pointi tatu za Toto ndiyo muhimu zaidi. Utaona kila mechi ni muhimu zaidi na presha inakuwa kubwa sana kila baada ya mechi moja.

“Wakati mwingine sitaki hata kuona mechi za Yanga kwa sababu ya presha kubwa, natamani kuona timu inashinda lakini ligi ni ngumu sana.

“Angalia pamoja na ubora wa kikosi cha Yanga, hakuna anayeweza kukataa kwamba tuna kikosi bora kabisa, lakini ushindi wetu sasa ni bao moja tu kwa mechi.

“Jiulize kwa nini tusishinde nne au tano, maana yake ushindani katika ligi ni mkubwa sana,” alisema Manji ambaye amekuwa kimya kwa muda mrefu.

Manji kwa kushirikiana na viongozi wenzake, wachezaji pamoja na wanachama na mashabiki wa klabu hiyo ameahidi kupambana ili kuhakikisha Yanga inakuwa bingwa mwishoni mwa msimu huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic