March 9, 2013




Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime ambaye hivi karibuni aliwahi kutoa ushauri wa kuwadhamini makocha wazalendo, ameshauri kusiwe na papara ya kuwatimua makocha wa kigeni na hasa wazungu.

Maxime ambaye alikuwa beki mahiri wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars, amekuwa akikiongoza vema kikosi chake ambacho kwa msimu huu kimekuwa kiboko ya Yanga na Simba.


“Ninaposema makocha wazawa wathaminiwe, sina maana wazungu au wageni wafukuzwe. Waendelee kuwepo na wanaweza kuwa sehemu ya changamoto.

“Lakini nasisitiza kuwe na tabia ya kuamini hata makocha wa Tanzania ni wazuri na kuna kila sababu ya kuwapima kutokana na kazi zao,” alisema Maxime.
Katika mechi zake nne za Ligi Kuu Bara katika mizunguko miwili, Mtibwa Sugar jumla ya pointi 10 huku kikiwa hakijapoteza hata mechi moja.

Katika mechi za mzunguko wa kwanza, Mtibwa iliifunga Yanga kwa mabao 3-0 na kusababisha kutimuliwa kwa aliyekuwa Kocha Mkuu, Tom Saintfiet. Mechi ya mzunguko wa pili, matokeo yakawa sare ya mabao 1-1 Yanga ikiwa chini ya Ernie Brandts.

Kwa upande wa Simba, mzunguko wa kwanza, Mtibwa Sugar iliichapa Simba mabao 2-0 na kusababisha tafrani kubwa kwa mashabiki kuandamana wakitaka nahodha Juma Kaseja na Geofrey Nyanga ‘Kaburu’ wajiuzulu.

Mechi ya mzunguko wa pili, safari hii Simba ikiwa na kocha mpya Mfaransa, Patrick Liewig ambalo linatamkwa Lievig, Simba ikalala kwa bao 1-0 na kusababisha presha kubwa ndani ya Msimbazi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic