March 9, 2013




Kama utani lakini dalili za jela zinanukia kwa mshambuliaji wa Manchester City, Carlos Teves ambaye amekamatwa akiendesha gari licha ya kuwa amezuiwa kuendesha kwa miezi sita.

Tevez raia wa Argentina alikamatwa karibu na kwake eneo la Alderley Edge, Cheshire akiendesha gari lake bila ya kujali Januari 6, mwaka alifungiwa kuendesha gari kwa miezi sita baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya barabarani.


Msemani wa Polisi wa Cheshire, Tevez mwenye miaka 29 alikuwa amezuiwa kuendesha gari kwa muda huo lakini amekamatwa tena na sheria inaonyesha adhabu yake ni miezi sita jela na fedha ya faini pauni 5,000.

Hata hivyo, Polisi baada ya kumshikilia kwa muda mchache, walilazimika kumuachia Tevez aendelee na mishe zake baada ya kutokuwa na mtu anayeweza kutafsiri kwa kuwa hawezi kuzungumza Kingereza.

Tevez anayejulikana kwa utukutu, ametakiwa kurejea Polisi Jumanne ijayo na ndiyo itajulikana kama atapelekwa mahakamani au anaweza kuepuka kifungo hicho hicho.

Mara baada ya Tevez kuzuiwa kuendesha gari, mara nyingi alionekana mitaani au hata mazoezini akiendeshwa na mkewe. Lakini baada akachoka na hali hiyo na kuamua kusukuma mwenye ‘mchuma’ wake.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic