March 7, 2013




Beki wa kati wa Yanga Ladslaus Mbogo aliyechana kiatu cha mshambuliaji Jerry Tegete kutokana na daruga lake, amesema yake ya moyoni.
Mbogo maarufu kama Mnyama kutokana na uchezaji wake wa kutumia nguvu au kutotaka mchezo hata mazoezini, amesema kiatu cha Tegete kimetengenezwa China.

Salehjembe iliamua kumsaka Mbogo ili aelezee namna alivyochana kiatu cha Tegete wakati wakiwa mazoezini juzi, hali iliyowashangaza wengi waliokuwa kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

 Mbogo (kulia) na Tegete...
Lakini yeye alisisitiza ilikuwa ni mchezo wa kawaida tu lakini kwa kuwa kiatu cha Tegete kimetengenezwa India, ilikuwa lahisi kuchanika.

“Aah, ilikuwa kawaida tu, sema huyu alikuwa amevaa kiatu kilichotengenezwa India,” alisema Mbogo mbele ya Tegete.

Tegete naye alijibu: “Usipoangalia huyu jamaa anaweza kukua, ni hatari sana. Kama kiatu kinachanika vile, binadamu itakuwaje.”

Tegete aliendelea kusisitiza huwa havai viatu feki lakini kazi ya Mbogo ni zaidi ile ya jeshi, hivyo akamuomba Mbogo apunguze madaruga kama ambavyo Kocha Ernie Brandts amekuwa akiomba.

Mbogo amesajiliwa na Yanga akitokea Toto African, ingawa hajapata namba kutokana na Yanga kuwa na mabeki wengi zaidi wenye uwezo, lakini ni kati ya wachezaji wazuri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic