March 6, 2013




Beki mpya wa kati wa Yanga, Ladslaus Mbogo amepewa jina la Myama na wachezaji wenzake. Anajulikana kuwa hataki mchezo mazoezini.


Mnyama hataki mchezo kweli, kwani hata mazoezini yeye anacheza kama yuko katika mechi na kama anakwenda kukaba, basi kila mmoja anahisi ni hatari.

Mara nyingi Kocha Mkuu, Ernie Brandts amekuwa akilazimika kusimamisha mazoezi na kumkumbusha beki huyo wa zamani wa Toto African kwamba apunguze nguvu ili asiwaadhibu zaidi wachezaji wenzake.

Kudhihirisha hilo, katika mazoezi ya jana ya Yanga, Mbogo alichana kiatu aina ya Adidas cha mshambuliaji Jerry Tegete.
Tegete alikutana na daruga la Mbogo na kuchana kiatu hicho. Tayari Tegete ameamua kununua kiatu kingine huku akisema Mbogo ni hatari sana.

“Kweli jamaa muacha aitwe Mnyama, angalia kiatu change. Jamaa kakimaliza kabisa, inabidi ninunue kingine,” alisema Tegete.

Juhudi za kumpata Mnayama ili azungumzie hilo bado zinaendelea ili kujua kweli kama ni mazoezi tu anachana hadi viatu, siku akipewa mechi, si ataua huyu?

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic