April 25, 2013



Beki wa kati wa Barcelona, Gerard Piqué amelazimika kubaki mjini Munich baada ya timu yake kuchapwa mabao 3-0 na wenyeji wao Bayern Munich.

Pique amebaki mjini humo kwa siku moja zaidi ili kufanyiwa vipimo kama anatumia dawa za kuongeza nguvu.

Taarifa zinaeleza vipimo hivyo vilifanyika juzi usiku na jana mchana, Pique aliondoka kurejea Hispania kuungana na timu yake.

Kumekuwa na utaratibu wa kuchagua wachezaji ambao wanapimwa kama wanatumia madawa ya kuongeza nguvu au la na yoyote anaweza kuchaguliwa kutoka kwenye timu moja au nyingine.

Katika mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa, Barcelona ilichapwa kwa mabao 4-0 na inalazimika kwenda kushinda 5-0 ili kusonga mbele.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic