April 25, 2013





Mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam sasa itafanyika Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Mabadiliko hayo yametokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetangaza kuahirishwa kwa mechi hiyo dakika chache zilizopita na kuomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza.

Hata hivyo, bado hali hiyo imewashangaza baadhi ya wadau kwamba TFF hawakuwa wakijua kwamba kutakuwa na maandalizi leo.

“Maandalizi ya muungano si kitu kigeni na siku ya muungano inajulikana kila mwaka, sasa vipi ijulikane leo,” alisema Mhariri wa Championi Ijumaa, John Joseph.

“Lakini kama haitoshi, angalau wangeahirisha jana ili watu wajue leo mapema, wanatangaza sasa saa saba kasoro mchana, maana yake wengine wako njiani wanakwenda uwanjani. Si kitu kizuri na inabidi waliangalie hili.”

Ligi hiyo inaendelea kesho (Aprili 26 mwaka huu) kwa mechi kati ya Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Jumapili (Aprili 28 mwaka huu) itakuwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni Simba dhidi ya Polisi Morogoro.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic