April 25, 2013



 
Pamoja na kuwa mmoja wa mashabiki wanaojitokeza mara nyingi Yanga inapokuwa inacheza Uwanja wa Taifa, Dar, muigizaji maarufu ameonekana kutojua lolote kuhusiana na suala la kusimama dakika moja ya kutoa heshima.


Kawaida kunapokuwa na mtu aliyepoteza maisha na anahusiana na soka au kiongozi wa serikali, mwamuzi hupuliza filimbi na watu uwanja mzima husimama kwa dakika moja ya kuomba na kuomboleza ikiwa ni sehemu ya heshima.

Lakini wakati Yanga inaivaa Ruvu JKT wiki iliyopita, pamoja na mwamuzi Oden Mbaga kuliza kipyenga kuashiria wakati wa kutoa heshima kwa marehemu Meja Jenerali Makame Rashid aliyekuwa mwanamichezo, Ray aliendelea kukaa kitako.

Pamoja na Ray, wasanii wengine wawili wa Bongo Movie, Chikoka na mwanadada Ketty waliendelea kubaki katika siti zao.


Lakini mchekeshaji, Steve Nyerere alionyesha kuchezwa na machale, akasimama na kuungana na wengine kumpa heshima marehemu.

Achana na Ray, mashabiki wengine wengi waliokuwa karibu na Ray walionekana kutolijua hilo, wakabaki vitini kimya, kitu ambacho si picha nzuri kwa maana ya michezo ni furaha na undugu pia.

Huenda Ray hakujua hili, lakini wakati mwingine anaweza asirudie kwa kuwa yeye kama kioo cha jamii anapaswa kuwa mfano.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic