Muda
mchache baada ya kuiangamiza Real Madrid kwa kufunga mabao manne, mshambuliaji
wa Borussia Dortmund, Robert Lewandowski
amekuwa ‘almasi’.
Klabu za
Bayern Munich na Manchester United wameanza kupita kila kona kuhakikisha
wanamnasa.
Mabao manne
aliyofunga dhidi ya Real Madrid, yamemfanya aweke rekodi ya kuwa mchezaji wa
kwanza kuifunga timu hiyo ya Hispania mabao manne katika mechi ya ligi ya
mabingwa.
Manchester
wangekuwa wa kwanza kumpata mshambuliaji huyo lakini Alex Ferguson akata kuwe
na subira.
Lakini
inaonekana Bayern ambao wameshabeba ubingwa wa Ujerumani kama ilivyo kwa Man
United England, ndiyo wenye nafasi ya kumnasa.
Huenda
mshambuliaji huyo raia wa Poland akachagua kubaki Ujerumani lakini akihama
kutoka mji wa Dortmund hadi Munich.
Iwapo Lewandowski
atakubali kujiunga timu kati ya hizo, atakuwa amebadili rangi ya jezi kutoka
njano na nyeusi hadi nyekundu na nyeupe.








0 COMMENTS:
Post a Comment