Pamoja na
sare Chelsea imejiweka katika nafasi nzuri ya kuingia nusu fainali ya michuano
ya Kombe la Europa Cup baada ya kuichapa FC Basel ya Uswiss.
Chelsea
ikiwa ugenini imepata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Waswiss hao ambao
watalazimika kushinda Stamford Bridge jijini London, wiki ijayo.
Chelsea
walipata bao lao katika dakika ya 12 baada ya Victor Moses kumalizia kona
iliyoguswa na Branislav Ivanovic.
Bao hilo
lilidumu hadi mapumziko lakini Basel walicharuka zaidi katika kipindi cha pili
kutaka kupata bao la kusawazisha lakini haikuwa hivyo.
Baadaye
Chelsea nusura wapate bao la pili baada ya shuti la Torres kugonga mwamba na
kurudi uwanjani na mabeki wa Basel wakaondosha hatari.
Basel
walipata bao la kusawazisha katika dakika ya 87 kupitia mkwaju wa penalti
uliopigwa na Fabia Schar, hata hivyo penalti hiyo ilionekana kulalamikiwa
kutokana na kuwa ya ‘magumashi’.
Wakati
mechi inaoneka inakwenda ukingoni, David Luiz alifunga bao la pili katika
dakika ya 90 kwa mpira wa adhabu.
Katika
mechi nyingine ya nusu fainali, Benfica ilikuwa ugenini dhidi ya Fenerbahce
ikiwa nyumbani nchini uturuki iliikaribisha Benfica ya Ureno.
Wenyeji
walifanikiwa kupata bao katika dakika ya 71 kupitia kwa Egemen Korkmaz na
Benfica wakaendelea kujitahidi kupata bao la ugenini.











0 COMMENTS:
Post a Comment