April 20, 2013





Baada ya mwezi mzima wa mapumziko kutokana na kufanyiwa upasuaji, hatimaye beki wa Yanga, Mbogo Ladslaus ameanza mazoezi na kikosi cha kwanza cha Yanga.


Mbogo ameanza mazoezi na wachezaji wenzake wa Yanga jana kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama, Dar es Salaam.


Wachezaji wa Yanga walionekana wenye furaha kubwa kumuona Mbogo akiwa amerejea uwanjani.


Mwenyewe Mbogo alionekana kuwa mwenye furaha na kabla ya kuanza mazoezi, alikutana na benchi la ufundi lililoongozwa na Kocha Mkuu, Ernie Brandts raia wa Uholanzi na kufanya majadiliano.

Baada ya majadiliano hayo, Mbogo aliruhusiwa kuingia mazoezini na kufanya na kuendelea na wenzake.
Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya alisema Mbogo atakuwa akifanya mazoezi ya taratimu hadi hapo atakapokuwa safi.


Awali ilielezwa kungekuwa na upasuaji wa pili katika shavu lake ili kuiweka sawa ngozi, lakini baadaye Matuzya amesema wataangalia hali yake inaendelea vipi.

Imeelezwa uvimbe alionao utakuwa unapungua taratibu na kwa muonekano wa leo, uvimbe huo wa shavuni umepungua kiasi ikilinganishwa na awali.

Mbogo alifanyiwa upasuaji wa shavu lake ili kuondoa uvimbe, hali iliyomlazimu kukaa nje ya uwanja kwa kipindi hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic