April 20, 2013



Baada ya msako mkali, hatimaye polisi wa Marekani wamefanikiwa kumnasa Dzhokhar Tsarnaev, 19, mtuhumiwa wa pili wa ulipuaji wa mabomu ya Houston Marathon.

Kijana huyo raia wa Chechnya alikamatwa jana usiku baada ya kukutwa amejificha katika boti katika eneo la Watertown nje kidogo ya Boston.


Tsarnaev alijificha kwenye boti na kaka yake baadaye akafichua siri, polisi walipofika katika eneo hilo akawa mbishi hivyo kufanya majibizano ya risasi yaanze kuanzia saa 1 usiku hadi saa 2:30 usiku aliponyoosha mikono.


Hata hivyo ilielezwa alinyoosha mikono baada ya kupigwa risasi mara mbili.


Baadaye alikamatwa damu zikiwa zinamvuja mwili mzima na akakimbizwa hospitali kwa matibabu na taarifa za awali zinaeleza alikuwa anatokwa damu nyingi sana.


Bado matibabu yanaendelea na wananchi wlaijitokeza mitaani kushangilia kuhusiana na mlipuaji bomu huyo ambaye pamoja na kaka yake aliishi Marekani tokea mwaka 2002.



Polisi walikuwa wakimkimbiza kwa takribani siku mbili baada ya kaka yake aliyekuwa mtuhumiwa wa kwanza kupigwa risasi na baadaye kufa akiwa hospitali.

Milipuko miwili karibu na sehemu ya kumalizia mbio hizo za Boston Marathoni ulisababisha watu watatu kupoteza maisha yao ikiwa ni pamoja na zaidi ya 100 kujeruhiwa wakiwemo 17 ambao walijeruhiwa vibaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic