April 21, 2013



 
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekalia kuti kavu katika nafasi yake hiyo.

Tayari kuna kikao kimefanyika kwa ajili ya kujadili kama Julio anaweza kubaki kuendelea kuinoa Simba au la.

Taarifa za uhakika ndani ya Simba zimeeleza kati ya vikao vilivyofanyika kujadili mambo kadhaa na mustakabari wa Simba, imeelezwa Julio alijadiliwa.

“Kweli tumemjadili Julio, inaonekana amekuwa akilalamikiwa karibu na kila upande, wachezaji wakongwe, chipukizi na hata benchi la ufundi.
“Amekuwa hana maelewano mazuri na karibu kila upande hali inayoonekana ni tatizo na inapoteza utulivu ndani ya timu,” kilieleza chanzo cha uhakika.

Hata hivyo Julio amekuwa Mbogo na asiyependa kuzungumzia mustakabari wake.

Katika majadiliano hayo, swali limekuwa ni kwamba Julio aondoke kabla ya msimu kwisha au baada.

Wako wanaounga mkono aondoke kabla lakini wengine wanataka aachwe hadi Simba itakapomalizika msimu kwa kuwa haina nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.

Hivi karibuni Julio alinuniana na bosi wake, Patrick Liwig hali ilizorotesha utendaji wa kazi wa benchi la ufundi.



Hata hivyo upande mwingine umeeleza kumekuwa na fitina zinazopikwa ili kumuondoa Julio katika nafasi yake kutokana na tabia yake ya kusema ukweli.
Julio amekuwa akiwaeleza wazi wachezaji wanaokosea hasa kuhusiana na suala la kutojituma mazoezini au kuitumikia timu kwammoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic