April 21, 2013



MADRID V BETIS
Pamoja na kwamba haina nafasi ya kutetea taji lake la La Liga, Madrid imeitandika Real Betis kwa mabao 3-1 huku mshambuliaji wake Mesut Ozil akifunga mabao mawili.


Bao moja lilifungwa na Karim Benzema na kuifanya Madrid izidi kujikita katika nafasi ya pili lakini ikaonekana ni kama mechi ya kujiandaa na Ligi ya Mabingwa hatua ya nusu fainali dhidi ya Borussia Dortmund. 


BARCA V LEVANTE
Barcelona nayo imezidi kujikita kileleni na kujihakikishia kwamba lazima iwe bingwa  La Liga baada ya kuichapa Levante kwa bao 1-0.

Cesc Fabregas aliyefunga bao hilo pekee huku ikionekana Barcelona si ile iliyozoeleka hasa kutokana na kumkosa mshambuliaji wake nyota Lionel Messi.


Mechi ngumu inafuatia kwa Barcelona ni ile ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya nusu fainali dhidi ya Bayern Munich.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic