April 29, 2013



Mashabiki na uongozi wa Queens Park Rangers umeonyesha kukasirishwa na kitendo cha beki, Jose Bosingwa kuonekana akicheka dakika chache baada ya timu hiyo kuteremka daraja.

Wachezaji na wadau wa QPR wamechukizwa na kitendo kinachomaanisha Bosingwa hakuumizwa hata kidogo na wao kuteremka daraja.


Picha zinamuonyesha beki huyo mwenye miaka 30 anayelipwa pauni 65,000 kwa wiki akicheka wakati anaingia vyumbani mara baada ya mchezo dhidi ya Reading ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana na kuidhinisha timu zote mbili kuteremka daraja.

Mashabiki wa QPR wameweka picha za Bosingwa katika mtandao wa kijamii wa Twitter akicheka kama ilivyokuwa kwa mchezaji mwingine, Clint Hill.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic