Wiki iliyopita, Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Kim Polusen
alitangaza kikosi cha pili cha timu hiyo ambacho kilichukua wachezaji kadhaa
waliokuwa wameonyesha uwezo wao katika mechi za Ligi Kuu Bara.
Wachezaji
wengi walioteuliwa na Poulsen ni wale waliokosa nafasi katika kikosi cha kwanza
cha Taifa Stars kutokana na ushindani mkubwa wa namba uliopo.
Wazo la
Poulsen ni zuri sana, huenda kama liliwahi kufanyika lakini kwa makocha lukuki
waliopita hawakuwahi kupendekeza suala hilo.
Kwanza
niseme ninampongeza Poulsen kutokana na wazo hilo, lakini pia Shikirisho la
Soka Tanzania (TFF) ambao wameona ni jambo la kiungwana na linaweza kuwa na
faida hapo baadaye.
Lakini kuna
kitu kingekuwa kizuri zaidi kwamba kwa vile katika benchi la ufundi la timu
kubwa, Poulsen ana wazalengo kama msaidizi wake, Sylvester Marsh na kocha wa
makipa, Juma Pondamali, basi ulikuwa wakati mzuri wa kufanya kazi na wazalendo
wengine.
Kwamba
badala ya kuendelea kukinoa kikosi hicho cha pili kwa kushirikiana na Marsh na
Pondamali, basi angeteua wazalendo wengi wawili ambao atafanya nao kazi. Mfano,
msaidizi wake anaweza kuwa Abdallah Kibadeni wa Kagera Sugar na Kocha wa Makipa
akawa, Ali Bushiri wa Zanzibar.
Hii
itasaidia mambo mengi sana, kwanza ni kwake Poulsen kuongeza wigo wa kufanya
kazi na makocha wazakendo, huenda akajifunza zaidi kuhusiana na uwezo wao.
Lakini
atajua mambo kadhaa kwa kuwa mfano Kibadeni ni kocha mkongwe na mwenye uwezo
mkubwa wa kung’amua vipaji vya wachezaji wa Kitanzania na kuna utuhibitisho wa
mambo mengi kama ilivyo kwa Bushiri ambaye amewahi kuitumikia Stars kwa
mafanikio makubwa ukiachana na kwamba alikuwa kipa mahiri enzi zake.
Haina maana
niliowataja mimi ndiyo wamepitishwa, walikuwa ni mfano tu. Lakini ukiachana na
Poulsen kufaidika, lakini taifa letu nalo litafaidika pia.
Tunakubaliana
kuwa Poulsen ni kati ya makocha wazuri wa kigeni ambao tumewahi kuwapata,
kufanya kazi na wazalendo maana yake analifadisha taifa letu kwa kuwa nao
watapata mambo kadhaa kutoka kwake.
Hivyo kama
katika kikosi kikubwa atakuwa na wazalendo tofauti na wale watakaokuwa timu B,
basi wigo wa faida utakuwa mkubwa zaidi kwa kuwa watakayojifunza, watayarudisha
katika timu zao na kufaidisa wengi zaidi.
Ukiachana
na hivyo, inawezekana kabisa siku moja Tanzania ikafikiria kuanchana na makocha
wageni na kuwaamini wazalendo ambao watakuwa ‘wamenyonya’ mambo kadhaa kutoka
kwa wageni na mwisho wakawa msaada kwa soka ya Tanzania.
Mwisho
niwapongeze waliochaguliwa katika kikosi hicho cha pili cha Taifa Stars.
Inawezekana kabisa walikuwa wakitamani siku moja kuichezea Taifa Stars kubwa na
hiyo ndiyo njia ya kufika huko.
Kitu
kikubwa wanachotakiwa kufanya ni kazi, waondokane na majungu, hisia tata na
ushabiki wa timu badala yake wafanye kazi ya kiushindani kwa ajili taifa na wao
wenyewe. Kila la kheri.








0 COMMENTS:
Post a Comment