April 19, 2013




Mkuu wa Idara ya Uanachama wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), Primo Carvaro ametua mjini Bujumbura, Burundi tayari kwa ajili ya kusuluhisha mgogoro.

Carvaro ametua mjini Bujumbura kimyakimya kusuluhisha mgogoro unaendelea katika shirikisho la soka nchini humo.

Hata hivyo, kumekuwa na hali ya kushangaza baada ya wanahabari kutojua lolote kuhusiana na kuwasili kwake nchini humo.

Ramadhani Kibuga, Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura ameiambia Salehjembe kuwa Carvaro ameongozana na watu wengine ambao hawajajua ni akina nani.

“Imekuwa ni kimyakimya ingawa kulikuwa na taarifa ya ujio wao, hivyo hatujui msafara wao una watu wangapi,” alisema.

Inaelezwa huenda ni ujumbe uleule uliotoka nchini siku chache na kufanya mahojiano na wagombea kadhaa walioenguliwa kwenye uchaguzi wa TFF wakiwemo Jamal Malinzi na Michael Wambura.

Wakati wakiwa nchini, baada ya kuwahoji wagombea wote waliokuwa wameenguliwa, Carvaro aliyekuwa ameongozana na Ashford Mamelodi walisema wanarejea Zurich, Uswiss katika makao makuu ya Fifa ambako wataliwasilisha suala hilo.


Walisema baada ya kuliwasilisha suala hilo, watakuwa na jibu kuhusiana na uchaguzi huo wa TFF na Carvaro alisisitiza halitakuwa jambo gumu kama linavyoelezewa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic