April 19, 2013



Mshambuliaji wa TP Mazembe, Mtanzania, Mbwana Ally Samatta amekuwa gumzo kubwa katika mechi ya kesho ya Ligi ya Mabingwa.
Mechi hiyo, TP Mazembe itakuwa na kazi ya kuwavaa wenyeji wake Orlando Pirates, timu yenye mashabiki wengi zaidi nchini humo.

Pirates na Mazembe zimekutana zaidi ya mara mbili tokea mwaka 2000 na zimekuwa na upinzani mkubwa.
Ndiaye..

 Lakini mashabiki wengi wa jiji la Johannesburg hasa Watanzania wamekuwa wakimzungumzia Samatta.

Kwa mujibu wa Mtanzania aitwaye John anayeishi jijini humo, amesema Samatta ndiye amekuwa kivutio zaidi.

“Unajua Pirates wanamtegemea Mzambia anaitwa Collins Mbesuma, lakini Wabongo na Wakongo hapa wanamzungumzia Samatta.
“Hata Mkongo mwenzao Tresor Mputu hawampi nafasi kubwa kama Samatta. Na hauwezi kuamini tiketi zimekatwa kwa wingi sana hapa kwa ajili hiyo.
“Watanzania wengi wanataka kwenda kumuona Samatta, maana baada ya kuwafunga Wamorocco mabao mawili amekuwa gumzo sana hapa,” alisema John.

Tayari Mazembe iko jijini Johannesburg na Kocha Mkuu, Lamine Ndiaye raia wa Senegal amesema mechi hiyo itakuwa ngumu na yenye ushindani wa juu.


Lakini akasisitiza amefurahishwa na wachezaji wake kuizoea haraka hali ya baridi huku akionyesha matumaini kwamba wameizoea haraka hali ya hewa.
Baridi imekuwa ikizidi kuwa kali nchini Afrika Kusini, awali Ndiaye alikuwa na hofu huenda ingeathiri kikosi chake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic