April 19, 2013


Bale

 Wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa msimu wa Ligi Kuu England (PFA) wametajwa.

Wachezaji sita wametangazwa kuwania tuzo hiyo akiwemo kiungo wa Man United, Michael Carrick ambaye hakutarajiwa.
 
Suarez
Wengine ni anayeshikilia tuzo hiyo, Robin van Persie, wengine ni Luis Suarez wa Liverpool, mshambuliaji nyota wa Spurs, Gareth Bale na viungo wawili wa Chelsea, Eden Hazard na Juan Mata. 

Hakuna beki wala kipa katika tuzo hiyo ambayo washindi hupatikana kwa wachezaji kupiga kura tofauti na ile nyingine ambaye mshindi hupatikana kutokana na wadhamini, msimu uliopita alishinda Vincent Kompany.
 
van Persie
Blogu ya Salehjembe imeamua kuchagua tatu bora yake na nafasi ya kwanza inakwenda kwa Bale, Suarez halafu van Persie huku wachezaji wawili wa Chelsea wakishika nafasi mbili za mwisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic