April 28, 2013



Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Pope amesema wamemkabidhi Kocha Mkuu, Patrick Liewig jukumu la kueleza mapungufu ambayo wao watayafanyia kazi.

Hans Pope amesema Liewig atawaeleza wao mapungufu na wachezaji katika nafasi gani wanatakiwa kusajiliwa ili kuwa na kikosi bora.
“Baada ya kocha kusema, basi sisi mara moja tutaanza kuyafanyia kazi na kama kusajili tutasajili.


“Kikubwa tunatoa nafasi kwa kocha aeleze anataka nini, baada ya hapo kazi yetu itakuwa ni kufanya usajili,” alisema Hans Pope ambaye alikubali kurejea Simba hivi karibuni.

Kati ya wachezaji wanaoonekana kukutana mapema na panga la Liewig raia wa Ufaransa ni mshambuliaji Mzambia, Felix Sunzu.

Tokea ametua Simba na kuchukua nafasi ya Milovan Cirkovic amekuwa akitumia kikosi cha vijana huku akiwa na mgogoro na wachezaji wengi wakongwe akiwemo Sunzu.

Sunzu ni kati ya wachezaji aliowasimamisha, lakini baadaye alirejea baada ya kukubali kuandika barua kuelezea sababu za msingi zilizomfanya atoweke kambini bila ya taarifa.

Kingine kitakachomuondoa Sunzu Simba, ni kutofanya vizuri msimu mzima huku akiwa analipwa kitita kikubwa zaidi cha mshahara cha dola 3,500 ambacho ni kikubwa zaidi kuliko anacholipwa mchezaji mwingine wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic