April 29, 2013



 
Wachezaji kadhaa maarufu wa Brazil amkiwemo Ronaldo, Bebeto walionekana kwa mara nyingine wakiwa uwanjani wakati wa ufunguzi wa Uwanja wa Maracana.


Uzinduzi wa uwanja huo ni baada ya ukarabati kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia na Michezo ya Olimpiki itakayofanyika mwakani nchini humo. 

Mechi hiyo ilikuwa ni kati ya marafiki wa Ronaldo na wale wa Bebeto na ilikuwa ni burudani kutokana na wachezaji wengi kuwa na maumbo makubwa lakini wakajitahidi kuonyesha makali.


Wakali hao walicheza mechi na kutoa burudani ya kutosha lakini nje ya uwanja huo kulikuwa na vita kati ya Polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga ubinafsishwaji wa uwanja huo kwa madai serikali itapoteza mapato.

Rais wa Brazil, Dilma Rousseff na Rais wa zamani wa nchi hiyo, Luiz Inacio Lula da Silva walikuwa kati ya watu 30,000 waliojitokeza katika uzinduzi huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic