April 30, 2013




Haikuwa kazi kwa Borussia Dortmund kutinga fainali ya Kombe la Uefa Champions League pamoja na kupoteza mechi kwa kufungwa bao 2-0 na wenyeji wake Real Madrid.

Cristiano Ronaldo na kocha wake Jose Mourinho waliokuwa na ndoto ya kufika fainali wakiwa na Madrid waliwashuhudia Dortmund walioshinda bao 4-1 katika mechi ya kwanza wakisonga kwa ulaini.



Kipindi cha kwanza kilikuwa na kosakosa kila upande na Madrid ndiyo walipoteza nafasi zaidi ya tatu za kufunga.

Lakini kipindi cha pili, Dortmund ndiyo walishambulia mfululizo likiwamo shuti la Lewandowski lililogonga mwamba.



Pamoja na kupoteza nafasi nyingi Madrid walipata mabao katika dakika ya 83 kupitia Sergio Ramos na dakika ya 88 mfungaji akiwa Sergio Ramos.
Madrid ilitakiwa ishinde kwa mabao 3-0 ili kusonga mbele, hivyo hadi mechi iliyochezeshwa na Muingereza Howard Webb inafika dakika 90, mabao 2-0 hayakuisaidia Madrid kusonga mbele zaidi ya kutengeneza heshima.

Michael Essien, Ramos, Angelo Di Maria, Benzema, Ozil walikuwa kati ya waliofanya vizuri lakini Ronaldo hakuwa na siku nzuri sana kutokana na kutocheza katika kiwango kizuri na kuisaidia timu yake kama ilivyotegemewa.


Kesho mechi nyingine ya nusu fainali itakuwa kati ya wenyeji Barcelona kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Camp Nou dhidi ya Wajerumani wengine, Bayern Munich.


Katika mechi ya kwanza mjini Munich, Barcelona walilala kwa mabao 4-0, hivyo wanalazimika kushinda 5-0 ili kusonga mbele.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic