April 20, 2013



 

Zimebaki saa chache kabla ya kiu ya Watanzania wapenda soka kukatwa.

Mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam FC na FAR Rabat ya Morocco itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar kuanzia saa 10 jioni.

Hata hivyo Azam FC inapaswa kuwa makini na mambo haya matano kutoka kwa Wamorocco hao waliowahi kuwa mabingwa.



Vichwa:
Wana sifa ya kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kupiga vichwa, maana yake Azam wanapaswa kuwa makini katika hilo.

Krosi:

Wana mawinga wazuri na wataalamu wa kuchonga krosi zenye macho, Azam wanabidi wazipe njia.

Kuchelewa:

Kwa kuwa wanacheza ugenini, watafanya kila wanaloweza kupata bao la mapema na baada ya hapo watapoteza muda na kushambulia mara chache kwa kushtukiza.

Kujilinda:

Wako ugenini, maana yake watajilinda sana na hawatataka nyavu zao ziguswe ili wakamalize kazi nyumbani.

Kujiangusha:

Wajanja sana wanapoingia katika eneo la hatari, wakiguswa tu wanajiangusha na kama refa ni wa mipango, basi mmekwisha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic