April 23, 2013


Amerudi...


Kiungo wa zamani wa Bolton, Fabrice Muamba hatimaye amerudi uwanjani na kucheza soka kwa mara ya kwanza baada ya kutofanya hivyo kwa takribani mwaka sasa.


Muamba alilazimika kustaafu soka kutokana na ugonjwa wa moyo ambao nusura uchukue uhai wake baada ya kuanguka uwanjani ghafla wakati wakiivaa Tottenham Hotspurs katika mechi ya Kombe la FA.

Baada ya kuanguka, moyo wa Muamba ulisimama kufanya kazi kwa saa 78, hali iliyozua hofu kubwa.

Lakini jana alirudi na kucheza mpira uwanjani tena lakini katika mechi za kujitolea kwa ajili ya kutoa misaada maarufu kama ‘Five aside’.
 
siku alipoanguka...
Muamba alionekana ni mwenye afya njema na kushirikiana na wenzake vizuri ingawa wapinzani wake walionekana kuwa na hofu kidogo.

Hata hivyo, Muamba alionekana kujiamini na kucheza soka vizuri huku dhahiri akionyesha alikuwa na hamu sana na soka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic