April 22, 2013



 
Mabao matatu aliyofunga Robin van Persie katika mechi dhidi ya Aston Villa yamemfanya aweke rekodi ya kuwa hat trick ya haraka zaidi tokea mwaka 2004.

Hat trick hiyo ya van Persie ndani ya dakika 33 tu imemfanya kuweka rekodi mpya tokea ile ya Mei 15, 2004 iliyowekwa na Mnigeria Yakubu Aiyegbeni wakati Portsmouth ilipokuwa inaivaa Middlesbrough.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu England, Portsmouth ilishinda kwa mabao 5-1, Mnigeria huyo akipiga mabao hayo matatu.



Pamoja na rekodi hiyo, van Persie amejiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa tena tuzo ya mchezaji bora wa mwaka, kwani amemzidi Suarez kwa bao moja katika listi ya wafungaji lakini ameisaidia United kutwaa taji la 20 la Ligi Kuu England.
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic