April 24, 2013



 

Pamoja na taarifa za kurejea tena wa Zacharia Hans Pope kufanya kazi za Simba, lakini baadhi ya wajumbe walioshiriki mkutano wa usuluhishi wameonyesha kuwa na hofu na utekelezaji wa mambo kadhaa waliyokubaliana.

Rage na baadhi ya wajumbe wa kundi la Friends of Simba wamekubaliana tena kufanya kazi pamoja katika mkutano ulioongozwa na Hans Pope ambaye pia alikuwa amejiuzulu.


Lakini mjumbe mmoja amesema mara kadhaa, Rage amewahi kuwageuka, hivyo wanataka kuona utekelezaji.

“Sisi hatukuwa na tatizo na utaona tulikubaliana mambo kadhaa ambayo yanatakiwa kutekelezwa kwanza. Tutasubiri kuona utekelezaji umefanytika.


“Imewahi kutokea mara kadhaa, utekelezaji ukawa shida na chairman (Rage) amekuwa hatekelezi mambo.

“Hivyo hatuwezi kusema kila kitu kimekamilika hadi utekelezaji utakapofanyika lakini sasa tunarudi kufanya kazi za Simba pamoja.

“Kitu kizuri hata Hans Pope naye amekubali kurudi, hivyo tutakuwa pamoja na tunachotaka kurekebisha mambo kadhaa na tumeomba tupewe nafasi,” alisema mjumbe huyo.

Taarifa zinaeleza, baada ya kuona mambo magumu, Rage aliamua kuomba kukutanishwa na maadui zake hao aliokuwa amewakoroga.

Hata hivyo nao waligawanyika kutokana na hofu ya kutoamini kama watakachokubaliana kitakuwa kauli dhabiti.

Lakini Hans Pope aliwahakikishia atalisimamia na kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri na alisisitiza alikuwa ameahidiwa na Rage kwamba kila kitu watakachokubaliana ndicho kutakwenda kama kilivyopangwa.

Simba sasa inawania nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi na inaonekana haina uhakika wa kuipata.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic