April 24, 2013




Mambo yanazidi kuwa magumu kwa mshambuliaji wa Liverpool, Luiz Suarez baada ya Shirikisho la Soka England (FA) kutangaza kumfungia mechi 10.

Kitendo cha kufungiwa mechi 10, maana yake Suarez ametoa nafasi ya mshambuliaji wa Manchester United, Robin van Persie kuwa mfungaji bora.


Pamoja na nafasi ya kuwa mfungaji bora kutoweka, lakini inaonekana hana nafasi tena ya kuwa mchezaji bora ambayo alikuwa anachuana zaidi na van Persie na Gareth Bale.
 


Van Persie anaongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 24, zaidi ya bao moja kwa Suarez mwenye mabao 23.

Suarez alikuwa anaongoza, lakini mabao matatu ya van Persie katika mechi dhidi ya Aston Villa imemfanya aongoze kwa bao hilo moja na kwa kuwa ataendelea kucheza ana nafasi ya kuongeza tena wakati Suarez hatacheza tena hadi mwisho wa msimu.

Liverpool na Man United, zote zimebakiza mechi tano za ligi, maana yake van Persie ana nafasi ya kuendelea kuongeza mabao.

Adhabu hiyo ni ya pili kwa Suarez, kwani tayari  amepigwa faini na Liverpool kutokana na kitendo cha kumng’ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic.

Kabla ya kutua England wakati anaichezea Ajax, Suarez aliwahi kumng’ata mchezaji wa timu pinzani, hali ambayo imekuwa ikiwashangaza wengi kutokana na tabia za ajabu za mshambuliaji huyo mbaguzi wa rangi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic