April 24, 2013


Julio na Liewig..


Uongozi wa Simba pamoja na kamati ya ufundi ya klabu hiyo umekaa na kujadili suala la wachezaji wapya.

Kikao hicho cha siri kimefanyika jijini Dar es Salaam na wachezaji kadhaa kutoka katika klabu mbalimbali wanaoonekana wanafaa wamewajadili.

Kamati ya ufundi ya Simba, imechukua mapendekezo ya kocha pamoja na mapendekezo yake na kuyajumuisha na kujadili pamoja na uongozi.


“Kilichojadiliwa ni wachezaji wapi wanaotufaa kwa ajili ya msimu ujao lakini tumeangalia mapengo, hasa nafasi zilizosumbua msimu huu,” kilieleza chanzo.

“Kidogo Simba kuna tatizo la fedha lakini kuanza kujadili mambo mapema ni suala la msingi halafu fedha zitatafutwa.”

Kati ya nafasi zilizokuwa tatizo ni beki wa kati, washambuliaji wawili namba tisa na kumi na hasa baada ya Mzambia Felix Sunzu kutofanya vizuri kwa takribani misimu miwili sasa.

Kocha Mfaransa, Patrick Liewig pamoja na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelo 'Julio' amekuwa akipendekeza kutumia vijana zaidi ingawa wazo hilo hakuwa amelianzisha yeye.

Uongozi wa Simba ulimuondoa Mserbia, Milovan Cirkovic na kumchukua Liewig lakini inaonekana mambo yalivyo ni ‘Leo, afadhari ya jana’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic