April 22, 2013





Uongozi wa Liverpool kupitia Ian Ayre umesisitiza utabaki upande wa mshambuliaji wao, Luis Suarez pamoja na kwamba alimuuma beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic.

Lakini imeelezwa pamoja na maneno hayo matamu ya Liverpool, kimyakimya imempiga faini Suarez kutokana na kitendo hicho walichokiita si cha kiungwana.



Suarez alimuuma Ivanovic wakati wakigombea mpira katika mechi ya Ligi Kuu England dhidi ya Chelsea ambayo ilimalizika kwa sare ya mabo 2-2, yeye akisababishwa moja walilofungwa Liverpool lakini akapoza machungu kwa kufunga la kusawazisha.


Suarez analipwa mshahara wa pauni 120,000 kwa wiki na faini aliyopigwa itakuwa kati ya zile kubwa zilizowahi kutokea ndani ya misimu mitatu ya EPL.

Taarifa kutoka ndani ya Liverpool zinaeleza, Suarez amepigwa faini kati ya pauni 200,000  na 400,000 ambao ni mshahara wake kati ya wiki mbili na tatu na utapelekwa katika vikundi vya kusaidia familia zenye matatizo.

Imeelezwa lengo la Liverpool kufanya mambo kwa siri ni kujaribu kupoza adhabu kutoka FA ambayo inaaminika lazima itamuadhibu.
Hata hivyo Ayre amesisitiza kwamba wataendelea kufanya kila linalowezekana kubadilisha tabia ya Suarez.

Lakini bado Liverpool imesisitiza, Suarez mwenye mtoto mmoja hatauzwa na ataendelea kubaki klabuni hapo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic