April 22, 2013



 
Muda mchache baada ya kupigwa faini na klabu ya Liverpool, mshambuliaji Luis Suarez ameziti kuingia matatani.

Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas ambayo  hutangazwa pia na Suarez imesema inalichukulia suala hilo kama kitu kikubwa.


Tayari imeshatoa taarifa ya kutofurahishwa na Suarez kumng’ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Anfield, Liverpool.

“Tutamkumbusha Suarez kiwango tulichojiwekea cha watu tunaotaka kufanya nao kazi na nini tunakuwa tunategemea kutoka kwao,” ilieleza taarifa kutoka Adidas na kufafanua zaidi.


“Tunafurahishwa na namna Liverpool wanavyolipeleka suala hilo, tunaamini wanakwenda vizuri. Luis amekubali alichokifanya si sahihi na tunaamini mambo yataenda vizuri.”

  Kitendo hicho cha Suarez kumng’ata Branislav Ivanovic kimechukua nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari dunia nzima na kufunika kabisa alichokifanya kusawazisha bao katika dakika za nyongeza na kufanya matokeo yawe sare ya mabao 2-2.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic