April 22, 2013




Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo anatarajia kutangaza wachezaji 30 vijana ambao watawania nafasi ya kucheza katika kikosi cha timu hiyo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zimeeleza, Poulsen atatangaza kikosi hicho kesho Jumanne na baada ya hapo timu hiyo itaingia kambini kwa siku kadhaa.

“Baada ya hapo, Poulsen atakaa kambini na vijana hao kwa siku kadhaa kwa ajili ya kuhakikisha anapata wengine wachache.


“Nimeambiwa huenda akachagua vijana watano ambao watapewa nafasi ya kucheza katika kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa.

“Poulsen ambaye amekuwa akifanya mazoezi na vijana hao kwa zaidi ya siku tano sasa, ameamua kufanya hivyo ili kupata vijana wengine baada ya akina Kapombe, Msuva kuanza kupata uzoefu,” kilieleza chanzo.

“Kocha anaamini vijana wanatakiwa, hivyo TFF wamekubali kusaidiana naye ili kumsaidia apate vijana wapya ambao pia watasaidia taifa.

“Kikubwa anachotaka ni vijana wenye vipaji ambao baadaye watakuwa msaada kwa taifa.”

Poulsen ambaye anaamini vijana, ameifanyia Stars mabadiliko makubwa katika kipindi chake na kuifanya iwe na kiwango cha kuvutia zaidi.

Kesho saa tano kamili, Poulsen atatangaza majina hayo pamoja na utaratibu mwingine wa namna kabi itakavyokuwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic