April 11, 2013



Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete anatarajia kuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya mechi tatu za timu hiyo ambazo ni muhimu zaidi.


Yanga ina mechi tatu muhimu ikiwemo ya kesho dhidi ya JKT Oljoro ambazo inatakiwa kushinda ili kutangaza ubingwa.

Kwa kuwa kila mechi ni dakika 90, iwapo Tegete atakosa mechi tatu maana yake atapoteza dakika 240 akiwa nje ya uwanja na Yanga ikipambana kupata ubingwa.


Tegete ambaye ni mmoja wa washambuliaji tegemeo wa Yanga, huenda akazikosa mechi zote kutokana na kusumbuliwa na maumivu makali ya goti.

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts amesema amelazimika kumpumzisha Tegete kwa muda ili kuangalia afya yake na hasa goti.

“Kutokana na ushauri wa daktari na nilivyoiona hali halisi, Tegete analazimika kupumzika. Ninaamini mechi tatu sidhani kama atacheza.

“Lakini kunaweza kukaw ana mabadiliko akarudi kucheza, hivyo ni suala la kusubiri na kumuombea apone haraka,” alisema Brandts, beki wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi.

Kwa zaidi ya siku nne au tano, Tegete amekuwa akionekana katika mazoezi ya Yanga lakini akiwa na nguo za nyumbani. 

Mshambuliaji huyo alianza kurudisha makali yake katika kupachika mabao lakini suala la majeruhi limeonyesha kumrudisha nyuma.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic