April 15, 2013



 Wachezaji nyota wa Ligi Kuu England akiwemo Rio Ferdinand wa Manchester United, wametapeliwa nchini Morocco.

Ferdinand, beki wa Chelsea ni kati ya wachezaji wanaokipiga katika Ligi Kuu England waliokuwa katika ujenzi wa nyumba za kisasa katika moja ya fukwe maarufu nchini Morocco.


Ujenzi we nyumba hizo ambao unaelezwa kutarajiwa kugharimu pauni milioni 200 (Sh bilioni 500) ungemalizika mwaka 2010, lakini hadi leo hakuna kilichofanyika.

Wachezaji hao wawili nyota wakiwemo wawili tena, Garry Neville aliyestaafu na Michael Carrick ambaye anakipiga Man United walishatanguliza ‘advance’ kwa ajili ya ujenzi huo, lakini hakuna nyumba hata moja iliyojengwa hadi leo katika eneo hilo.

Eneo hilo lingekuwa na nyumba zipatazo 1,342 pamoja na viwanja vitatu vya mchezo wa gofu, viwanja vya michezo mbalimbali pia.

Terry, Rio na wenzake wamekuwa wkaitumika katika matangazo ya ujenzi wa eneo hilo maarufu kama Le Jardin de Fleur katika eneo la Saidia, ili kuwashawishi watu wajitokeze na kulipa fedha kwa ajili ya kujengewa nyumba.


Wachezaji hao wameendelea kuwa kimya lakini Mkurugenzi wa Developer Property Logic inayoshughulikia ujenzi huo, Sean Cusack amesema bado wana imani ya kumaliza ujenzi huo.

“Hakuna aliyetegemea kilichotokea, lakini tunaamini mambo yatakuwa mazuri na wanaotaka nyumba au waliolipia watapa wanachotaka. Tulipata matatizo ya kifedha ambayo yalitokea dunia nzimba,” alisema.
Inaaminika mnamo mwaka 2006, Developers Property Logic walikusanya pauni milioni 40 kutoka kwa waliokuwa wanataka nyumba katika eneo hilo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic